MAPISHI - Visheti

visheti


 
VIPIMO:

Unga wa Visheti

Unga                                        4 Vikombe vya chai

Siagi                                        1 Kikombe cha chai

Hiliki                                        ½ Kijiko cha chai

 

NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA

1. Tia unga kwenye bakuli pamoja na siagi na hiliki.

2. Changanya vizuri isiwe na madonge.

3. Tia maji baridi vikombe viwili kasoro vya chai changanya ukiona bado ongeza maji kidogo, iwe kama chapati usikande uchanganye tu.

4. Halafu utakata sampuli  unayopenda mwenyewe.

5. Unaweka karai ya mafuta yakisha kupata moto unaanza kuchoma moto usiwe mkali sana, kiasi, baadae unaweza kuongeza moto na vikaange    hadi viwe rangi ya dhahabu, kisha viepue vichuje mafuta. .

6.  Ukipenda gawa visheti sehemu mbili, na shira pia igawe sehemu mbili

7. Changanya nusu ya visheti kwa shira nyeupe.

8. Nusu ya shira nyingine ibandike tena motoni na tia cocoa vijiko viwili vidogo vya chai. Inapochanganyika cocoa vizuri changanya  nusu ya visheti ulivyogawa kupata visheti vya shira ya cocoa.

 Shira:

Sukari                                    2 Vikombe vya chai

Maji                                       1 Kikombe cha chai

Vanilla                                    ½ Kijiko cha chai

(cocoa ukipenda kugawa visheti aina mbili) 2 Vijiko vya chai.









MAPISHI :  Je unapenda kupika lakini hujui? kama jibu ndio basi karibu sana katika page hii ya mapishi ambayo utapata machache ambayo yatakusaidia katika masuala mazima kuhusu kupika.

Powered by Pnyxe








Free Web Hosting