MAPISHI - Pilau Ya Nyama Ya Ng'ombe Na Nyanya 

dd


 
 Vipimo

 Mchele (Basmati)                                          3 vikombe

 Nyama ya ngo’mbe                                      1 kg

 Pilipili boga                                                    1 kubwa

 Nyanya                                                        2 kubwa

 Vitunguu maji                                               2 vikubwa

 Thomu iliyosagwa                                         1 kijiko cha supu

 Tangawizi                                                     1 kijiko cha chai

 Ndimu                                                          1

 Mafuta ya kupikia                                         ½ kikombe

 Mdalasini                                                      ½  kijiko cha chai

 Binzari nyembamba                                      1 kijiko cha chai

 Pilipili manga                                                  ½ Kijiko cha chai

 Hiliki                                                             ½ Kijiko cha chai

 Namna ya kutayarisha na Kupika

 1. Roweka mchele wako katika chombo

2. Chukuwa nyama na ioshe vizuri na itie thomu, tangawizi, ndimu, pilipili manga na chumvi kiasi

 3. Iweke jikoni hadi ikauke maji na kuwa imewiva huku ukiikaanga kaanga kwa hayo hayo mafuta yake hadi kuwa rangi ya hudhurungi

 4. katakata Vitunguu na nyanya weka pembeni

 5. Chukua pilipili boga, thomu, tangawizi na visage katika mashine ya kusagia

 6. Weka sufuria pembeni na utie mafuta, subiri yapate moto

  7. Kisha tia vitunguu na vikaange hadi kuwa hudhurungi na tia nyanya

  8. Kisha mimina mchanganyiko wako ulio usaga wa pilipili boga, thomu na tangawizi
 
9. Koroga kwa dakika kadhaa Kisha mininia nyama uliyokuwa tayari, maji kiasi na chumvi wastani na subiri maji hayo yachemke

 10. Weka mchele humo na koroga kiasi na onja chumvi kama ipo sawa au kama ndogo unaweza kuongeza

 11. Funika na punguza moto na uache uive taratibu

12. Baada ya kukauka maji kabisa basi ugeuze na subiri tena kwa dakika kama mbili na tayari kuliwa.




MAPISHI :  Je unapenda kupika lakini hujui? kama jibu ndio basi karibu sana katika page hii ya mapishi ambayo utapata machache ambayo yatakusaidia katika masuala mazima kuhusu kupika.

Powered by Pnyxe







Free Web Hosting