MAPISHI - Biskuti za jam

biskuti za jam


 
VIPIMO
 

Unga                                          2 ½ gilasi

Sukari                                        ¾ gilasi

Samli                                         1 gilasi

Mayai                                         2

Baking powder                            2 kijiko vya chai

Vanilla                                        1 ½ kijiko cha chai

Maganda ya chungwa                1
 
 
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA 
 
1.      Tia kwenye machine ya kusagia (blender) mayai, sukari, vanilla, samli na maganda ya chungwa, saga vizuri.
 
2.      Tia unga kwenye bakuli pamoja na baking powder, mimina vitu ulivyosaga kwenye bakuli, changanya.
 
3.      Punguza unga uliochanganya kidogo weka pembeni.
 
4.      Unga uliobakia tia kwenya tray ya kuchomeya, utandaze vizuri, tia jam juu yake.
 
5.      Chukua la kukwaruzia carrot (grater) ukwaruze unga uliuopunguza juu ya jam.
 
6.      Choma kwa muda dakika 20 moto wa 180 C.
 
7.      Acha ipowe kidogo, zikate vipande vya mraba (square) Tayari kwa kula..









MAPISHI :  Je unapenda kupika lakini hujui? kama jibu ndio basi karibu sana katika page hii ya mapishi ambayo utapata machache ambayo yatakusaidia katika masuala mazima kuhusu kupika.

Powered by Pnyxe








Free Web Hosting